Je, Toto inaweza kutimiza ndoto za kurudi ligi kuu
kwa staili hii?
Thursday, September 18, 2014
Wednesday, September 17, 2014
MAKALI YA DANNY WELBECK BADO
MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck jana
alikuwa ana nafasi nzuri ya kuwa shujaa wa timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa
hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund, lakini
akashindwa kuitumia.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 16
kutoka kwa wapinzani, Manchester United jana alienedelea kupewa nafasi katika
kikosi cha kwanza cha The Gunners na kocha Arsene Wenger akionyesha alimsajili
kwa sababu alimuamini, lakini akashindwa kuwafurahisha mashabiki.
Muingereza huyo jana alipata nafasi tatu nzuri za
kuifungia Arsenal mabao kuanzia mapema kipindi cha kwanza, lakini zote
akashindwa kuzitumia, The Gunners wakichapwa mabao 2-0 na Dortmund ugenini.
UBAGUZI WA RANGI WAENDELEA KURINDIMA
Friday, July 18, 2014
Nafaka bingwa kombe la polisi jamii
Timu ya Nafaka Fc ya wilayani Misungwi mkoani Mwanza imejitwalia ubingwa katika mashindano ya polisi jamii kwa kuifunga Muungano Manawa fc kwa mikwaju ya penati 8-7, baada ya ushindi wa bao 1-1.
POLISI, WAANDISHI WA HABARI KUPATIWA MAFUNZO YA MILIPUKO
Kutokana na kuongeza kwa milipuko ya mabomu nchini ambayo imekuwa ikileta madhara hasa kwa waandishi wa habari na askari polisi, chuo cha Dar es Salaam cha uandishi wa habari na mawasiliano ya umma (DIJM) kupitia tawi lake la jijini Mwanza, kinatarajia kutoa mafunzo maalum kuanzia August 11 mwaka huu.
Subscribe to:
Posts (Atom)





