Thursday, September 18, 2014

Wednesday, September 17, 2014

NGASSA BADO NYOTA INA NG'AA


MAKALI YA DANNY WELBECK BADO



MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck jana alikuwa ana nafasi nzuri ya kuwa shujaa wa timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund, lakini akashindwa kuitumia.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 16 kutoka kwa wapinzani, Manchester United jana alienedelea kupewa nafasi katika kikosi cha kwanza cha The Gunners na kocha Arsene Wenger akionyesha alimsajili kwa sababu alimuamini, lakini akashindwa kuwafurahisha mashabiki.



 Muingereza huyo jana alipata nafasi tatu nzuri za kuifungia Arsenal mabao kuanzia mapema kipindi cha kwanza, lakini zote akashindwa kuzitumia, The Gunners wakichapwa mabao 2-0 na Dortmund ugenini. 

UBAGUZI WA RANGI WAENDELEA KURINDIMA


Mwanasiasa huyo kutoka chama cha PAN amembagua Ronaldinho akimfananisha na sokwe.
Sababu kubwa ya kumbagua ni kutokana na foleni kubwa ya magari barabarani iliyosababishwa na mashabiki wa timu ua Querétaro aliyojiunga nayo nchini Mexico.
Wengi walikuwa wanatokea uwanjani wakati Ronaldinho anatambulishwa.
Mwanasiasa huyo akaamua kuandika kwenye ukurasa wake wa Facebook, kama anachukizwa na mchezo wa soka na anashangazwa watu kusababisha foleni sababu ya sokwe mmoja.
Kauli hiyo ilipingwa na wengi na kusababisha mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri kuifuta post yake.
Hata hivyo, watu wameendelea kumsakama na kupinga kitendo chake hicho cha kibaguzi.


Friday, July 18, 2014

Nafaka bingwa kombe la polisi jamii

Timu ya Nafaka Fc ya wilayani Misungwi mkoani Mwanza imejitwalia ubingwa katika mashindano ya polisi jamii kwa kuifunga Muungano Manawa fc kwa mikwaju ya penati 8-7, baada ya ushindi wa bao 1-1.

POLISI, WAANDISHI WA HABARI KUPATIWA MAFUNZO YA MILIPUKO


Kutokana na kuongeza kwa milipuko ya mabomu nchini ambayo imekuwa ikileta madhara hasa kwa waandishi wa habari na askari polisi, chuo cha Dar es Salaam cha uandishi wa habari na mawasiliano ya umma (DIJM) kupitia tawi lake la jijini Mwanza, kinatarajia kutoa mafunzo maalum kuanzia August 11 mwaka huu.

HAPA UTAIPENDA RAMADHANI