Tuesday, September 23, 2014

Wednesday, September 17, 2014

NGASSA BADO NYOTA INA NG'AA


MAKALI YA DANNY WELBECK BADO



MSHAMBULIAJI mpya wa Arsenal, Danny Welbeck jana alikuwa ana nafasi nzuri ya kuwa shujaa wa timu hiyo katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Borrusia Dortmund, lakini akashindwa kuitumia.
Mchezaji huyo aliyesajiliwa kwa Pauni Milioni 16 kutoka kwa wapinzani, Manchester United jana alienedelea kupewa nafasi katika kikosi cha kwanza cha The Gunners na kocha Arsene Wenger akionyesha alimsajili kwa sababu alimuamini, lakini akashindwa kuwafurahisha mashabiki.



 Muingereza huyo jana alipata nafasi tatu nzuri za kuifungia Arsenal mabao kuanzia mapema kipindi cha kwanza, lakini zote akashindwa kuzitumia, The Gunners wakichapwa mabao 2-0 na Dortmund ugenini. 

UBAGUZI WA RANGI WAENDELEA KURINDIMA


Mwanasiasa huyo kutoka chama cha PAN amembagua Ronaldinho akimfananisha na sokwe.
Sababu kubwa ya kumbagua ni kutokana na foleni kubwa ya magari barabarani iliyosababishwa na mashabiki wa timu ua Querétaro aliyojiunga nayo nchini Mexico.
Wengi walikuwa wanatokea uwanjani wakati Ronaldinho anatambulishwa.
Mwanasiasa huyo akaamua kuandika kwenye ukurasa wake wa Facebook, kama anachukizwa na mchezo wa soka na anashangazwa watu kusababisha foleni sababu ya sokwe mmoja.
Kauli hiyo ilipingwa na wengi na kusababisha mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri kuifuta post yake.
Hata hivyo, watu wameendelea kumsakama na kupinga kitendo chake hicho cha kibaguzi.